Header Ads

Kutoka Zanziber: BOMU LA MISUMARI LAUWA MMOJA ZANZIBAR

Bomu la misumari lauwa mmoja Zanzibar

 14 Juni, 2014 - Saa 12:23 GMT

MJi mkongwe, Zanzibar
Mtu mmoja ameuwawa huku wengine kadhaa kujeruhiwa katika shambulio la bomu kisiwani Zanzibar.
Baadhi ya waathiriwa walikuwa wanaondoka katika msikiti mmoja ulioko katika maeneo ya mji mkongwe, mjini Zanzibar.
Haijulikani ni nani aliyefanya shambulio hilo ambalo lilijiri mkesha wa sherehe za kimataifa za filamu katika kisiwa hicho; na piya wakati kuna kongamano ya viongozi wa dini ya Islamu katika Afrika Mashariki, likifanyika huko.
Mwandishi wetu nchini Tanzania amezungumza na Insepekta Mkuu wa Zanzibar, Mohammed Mhina, ambaye amemwambia kuwa bomu liloripuka lilikuwa na misumari.

Hilo ni shambulio la pili la bomu mwaka huu.
Mwezi February mabomu mawili tofauti yaliripuliwa nje ya kanisa Anglikana, mji mkongwe, pamoja na mkahawa uliokuwa karibu na kanisa hilo.
Kumekuwa na hali ya wasiwasi wa kidini katika kisiwa hicho.

ANGALIA PICHA INASIKITISHA; BOMU LALIPUKA DARAJANI ZANZIBAR, MMOJA AFARIKI


 Mlipuko unaosadikiwa kuwa ni bomu jana Juni 13, 2014 ulilipuka eneo la Darajani Zanzibar na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi watatu.
Tarifa zinasema mlipuko Huo umetokea baada ya waumini wa dini ya kiislamu kumaliza muhadhara uliokuwa ukitolewa Miskiti wa darajani baada ya salsa ya Isha.
Aliyekufa ni mmoja kati ya wahadhiri waliokuja kutoka Tanga na Sheikh Hamad ndiyo aliyekuwepo theater. Na Sheikh Kassim Mafuta kaumia kidogo.
Majeruhi 3 wamelazwa hospitali ya Mnazi Mmoja, Zanzibar wakiwa na majeraha madogo 'madogo. Majeruhi wa nne yupo theatre sasa hivi na nali yake sio mbaya

No comments

Powered by Blogger.