KUHUSU ILE ISHU YA MWANAMKE ALIYEFANYA MAPENZI NA SAMAKI DOLPHIN
Jumatano, Juni 11, 2014
Unaweza kushangaa na kuona ni kitu cha ajabu lakini hii imetokea
ambapo mwanamke ambaye alifanya mapenzi na samaki aina ya Dolphin ikiwa
ni sehemu ya utafiti wa kisayansi amezungumza kwa mara ya kwanza juu ya
hatua hiyo.
Mwanamke huyo Margaret Howe Lovatt ambaye ni mtafiti wa wanyama
amesema alikuwa sehemu ya utafiti huo uliofanyika katika kisiwa cha
Virgin nchini Marekani kwa ajili ya kuwafundisha viumbe wa baharini
wenye akili jinsi ya kuongea kiingereza.
Margaret Howe Lovatt
anasema alikuwa akijaribu kumfundisha Peter (the dolphin) jinsi ya
kuongea kiingereza lakini uhusiano wao ulikwenda mbali zaidi.
Ilikuwa mnano wa mwaka 1963 ambapo walimsaidia kutengeneza bwawa la
Dolphin nyumbani kwake ambako wanasayansi wangeweza kuwasoma wanyama hao
wakiwa nyumbani, ndipo hapo Margaret alipokuna na Peter ambaye ni
samaki aina ya Dolphin kwa wakati huo akiwa bado mdogo ambapo wawili hao
wakapatana na mahusiano yao kukua zaidi kimwili.
Margaret amenukuliwa akisema kuwa
Peter (Dolphin) alipenda kuwa na mimi, mara nyingi alikuwa akijisogeza mwenyewe karibu yangu kwenye mguu wangu au mkono na kuruhusu kitendo hicho.Haikuwa shida kwangu kwani Peter alikuwa akihisi uwepo wangu na kuona ni kitendo cha kimapenzi kwa upande wake lakini kwangu niliona ni kitu cha kawaida kama sehemu ya masomo yangu.
Post a Comment